Application Form for Academic Year 2024/2025.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tanzanian Training Centre for International Health, (TTCIH) anawatangazia umma nafasi za kujiunga na chuo kwa mwaka wa masomo 2024/2025. TTCIH ni taasisi ya mafunzo ya Afya Ifakara iliyosajiliwa na NACTVET kwa namba HAS/003, Chuo kipo Ifakara mjini, Mkoani Morogoro. Chuo kina mazingira tulivu na mazuri kwa kujifunza ikiwa pamoja wakufunzi wabobezi katika masomo yote, Hospitali ya kujifunzia, maktaba bora na masomo kwa njia ya kielektroniki yaani eLearning.

Chuo Kinatoa Kozi Zifuatazo

  1. Stashahada ya Utabibu (Diploma in Clinical Medicine) – Miaka Mitatu
  2. Stashahada ya Utabibu ya Mwaka Mmoja (Yaani upgrading from Clinical Assistant to Clinical Officer).
  3. Stashahada ya Ufamasia (Diploma in Pharmaceutical Sciences) – Miaka mitatu
  4. Stashahada ya Optometria (Diploma in Optometry) – Miaka mitatu

Sifa za Mwombaji kwa Kozi ya Stashahada ya Utabibu ya Miaka Mitatu awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Chemistry na Physics

Sifa za Mwombaji wa Stashahada ya Utabibu Mwaka Mmoja (Yaani Upgrading From Clinical Assistant to Clinical Officer ) awe :

  • Amehitimu Astashahada ya Utabibu (Technician Certificate in Clinical Medicine).

Sifa za Mwombaji kwa kozi ya stashahada  ya Ufamasia (miaka mitatu) awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufaulu wa angalau D ya Biology na Chemistry

Sifa za Mwombaji kwa kozi ya stashahada  ya Optometria (Miaka mitatu) awe :

  • Amehitimu kidato cha nne kwa ufualu wa angalau D ya Biology, Chemistry, Basic Mathematics, English  na Physics/Engineering Sciences

Jinsi ya Kujaza Fomu za Maombi

Maombi yote ya kujiunga na Chuo yanatumwa kupitia tovuti ya NACTVET  kwenye kiunganishi (QUICK LINK ) kilichoandikwa MAOMBI YA UDAHILI VYUO VYA AFYA 2024, Kwa msaada wa kujaza FOMU MOJA KWA MOJA CHUONI, tafadhali jaza taarifa zako kwenye hii fomu hapa chini  kisha bofya “SEND” dawati la usajili litakupigia simu  muda wowote kukusaidia kujaza fomu kikamilifu au piga simu namba zifuatazo (+255) 0718365374, 0718 552 164, 0758943044 & 0710527003 

KARIBU TTCIH IFAKARA KWA MAFUNZO YENYE KUJENGEA WAHITIMU UWEZO KUTOA TIBA KWA KUTUMIA TAFITI YAANI  EVIDENCE BASED MEDICINE

Our Clients Reviews & Testimonials